Viongozi wa Umoja wa Afrika wamemteua rais Robert Mugabe wa
Kiongozi huyu mwenye miaka 90 amekabidhiwa wadhifa huo na Rais wa
Mauritania ,Mohamed Ould Abed Aziz ambaye alikuwa mwenyekiti hapo awali.
Viongozi hao wa Afrika, wakiongozwa na rais wa Uganda Yoweri
Museveni pia watajadilia mkakati wa kujiondoa kwenye uwanachana wa
Mahakama ya Kimataifa ya jinai-ICC.
Akizungumza na waandishi habari hapo awali jijini Nairobi, rais
huyo wa Uganda alisema “Mahakama hiyo ya Wazungu inaendelea kuonyesha
ujeuri na dharau kwa Waafrika.” Alisema ingawa ICC imeondoa kesi dhidi
ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, bado hajaridhika kwa sababu kesi
dhidi ya Naibu rais wa Kenya William Ruto ingali inaendelea.
Wakati huo, huo viongozi hao wa Afrika wameidhinisha mpango wa
kupeleka kikosi cha pamoja cha wanajeshi 7,500 cha kukabiliana na
wanamgambo wa Boko Haram.
Hatua hiyo imefikiwa wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kila mwaka wa
Umoja wa Afrika uliofanyika Addis Ababa mji mkuu wa Ethiopia Ijumaa .
Nchi za Nigeria , Cameroon,Chad, Niger na Benin zilikubaliana
kushirikana katika juhudi za kukabiliana na wanamgambo hao ambao wameua
maelfu ya raia huko Nigeria na kujinyakulia eneo kubwa la jimbo la
Borno karibu na mpaka wa Cameroon na Chad.
0 maoni:
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.