Na Hosea Mchopa #UO 1
.Hii si habari kubwa kwenye ulimwengu wa Mario Balotelli,hata
akiangalia video ya Steven Gerrad akimkosoa anaweza akapata kicheko kikali.Kipi
Mario kinamumiza kichwa kama anasakamwa na dunia nzima kumwacha mama yake aishi
katika maisha ya kawaida wakati yeye akichezea madola.
Mama yake mzazi Rose Barwuah anatazama maisha ya kimilionea
ya mwanae wa kumzaa kama wewe unavyotazama.Mama yake anaishi maisha ya kawaida
kabisa Wythenshaw pale Manchester.Mama yake kwa upendo alionao kwa Mario
alihamia mjini Manchester ili kuwa kwa karibu na mwanae kujenga mahusiano bora
baada ya Mario kuhamia Manchester City.
Familia nzima ya Mario Barwuah Ballotelli
Mama yake Mario Balotelli amezoea shida kama waafrika wengine
wanavyoishi ulaya.Anatengeneza pesa kwa kufanya usafi kwenye majumba ya watu na
popote pale penye uhakika wa kumuingizia pesa.
Wakati Mario Ballotelli anaishi kwa kufanya chochote
apendacho katika dunia hii akiendesha Ferrari F12 Berlineta lenye gharama ya
paun 240,000.Muda wa chakula ukifika ana uwezo wa kwenda kula mighahawa ya
gharama katika jiji la Liverpool.Mama yake bado anapanda mabasi ya abiria na
mahitaji yake anachukua maduka ya kawaida kabisa.
Mama yake Rose na dada yake mwenye maiaka 15 Angel wanaishi
kawaida sana wanachohitaji ni upendo tu kutoka kwa damu yao.Pesa zake sio kitu
muhimu katika maisha yao.Enoche ndio binadamu pekee ambaye Mario Balotelli uwa
nae karibu ambaye anacheza katika klabu
ya Vallecamonica.
![]() |
Balotelli na Enoche wakifurahi picha |
![]() |
Balotelli akiwa na Enoche enzi za utoto wao |
Mario Balotelli damu yake tu ndio ya mzee Thomas Barwuah na
Rose Barwuah lakini yeye ni mali halali
ya Silvio na Francesco Balotelli waliyekabidhiwa akiwa na miaka 2.Na kuishi nao
huku siku za jumapili akipata nafasi ya kujumiaka na Enoche na familia kwa
ujumla.Mario alilelewa kwa heri na wazazi wake hadi hali yake ilipokuwa mbaya
ikabidi wazazi watafute sehemu itakayokuwa inampa uhakika wa kuweza kuishi
maana daktari alisema anaweza akapoteza maisha.
![]() |
Mario Balotelli akia na mdogo wake Enoche na mama yao Rose Barwuah |
Ushahidi wa picha za pamoja unaonesha Mzee Barwuah hakumtupa
na wala haitaji pesa zake kama Mario alitomka.Anakumbuka tabasamu lake udogoni
akicheza mpira katika mvua na kumwita Super Mario.Na sasa akiwa Mario mwingine
kabisa anayeamini pesa ndizo zinaifanya famillia imkumbuke japo kwa sasa
anajirudi kiasi.Hii si habari kwangu na wala haitaingia katika kumi bora zangu
za Mario nitakumbua hivi tu.
![]() |
Balotelli akiwa na wazazi wake waliomwasili Silvio na Francesco |
Ilikuwa dakika ya 85 mechi kali ya kombe la ulaya kati Liverpool na Besktas.Mwanaume
mwenye kilo 86.17 anachukua mpira na kwenda kupiga penati pasipo nahodha wa
timu Hendo kumruhusu kwa moyo mkunjufu.Anafunga
penati na kuipa matokeo Liverpool matokeo muhimu katika uwanja wa Anfield.
Mario Balotelli akijiandaa kupiga penati
Hana shaka lolote katika hii sayari mawazo yake yako haraka
kufanya maamuzi ya ajabu ambayo kwake yanakua sahihi kwa huo mda.Unakumbuka
alipomuuliza mdogo wake Noche unataka kuona wafungwa.Na ghafla akaelekeza gari
ndani katika gereza la wanawake Italia.
Manung’uniko humalizwa na furaha,na hakuna furaha tamu kama
ile ya kushitukizwa.Henderson Jordan alisahau kama Super Mario alifanya
kosa.Furaha hii imefanya mashabiki wa Liverpool wasielewe kabisa lugha
anayoongea kipenzi chao cha miaka mingi Steven Gerrad.
![]() |
Balotelli akishangilia baada ya kufunga peanti dakika ya 85 |
Steven Gerrad akiongea katika kituo cha televisheni Uingereza
ITV aliongea kwa msimamo kuwa Mario Balloteli ameonesha kitendo cha utovu wa
nidhamu kwa Jordan Henderson.Gerrad alichukizwa na kitendo cha Mario Balloteli
kwenda kupiga penati na kumpora mpira Henderson wakati alikuwa tayari kwenda
kupiga penati.
Kocha Brendan Rogers kwa upande wake yeye alisema ni matokeo
mazuri na wanajipanga kwa mchezo wa marudiano.Hakuwa na pingamizi kwa
yaliyotokea matokeo ya ushindi ndiyo yalikuwa jambo la muhimu kwake.
Ingawa baadae akiongea na waandishi wa Habari katika
maandalizi ya mchezo wa jumapili alisema hakupendezwa na namna wachezaji wake
walivyokuwa wanamgogoro juu ya nani atapiga penati.Henderson ndiye alimpanga
mbadala wa Gerrad kupiga penati katika kikosi kilichoanza.
Kwa kawaida kama Gerrad,Henderson na Mario wapo ndani wote
wameanza.Mario na Gerrad ndio huwa wananafasi kubwa ya kupiga penati.Kwa kuwa
Mario hakuanza mechi basi Henderson ndiye alistahili kupiga penati.
Pamoja na haya hakuna
cha kupoteza katika maisha ya Mario Balotelli amefunga goli lake la nne kwa
msimu na la pili kwa kombe la ulaya.Ametengenza historia tamu ya kipekee
kufunga penati 26 kati ya 28 alizopiga.
Jordan Henderson ambaye alikuwa kiongozi wa wachezaji katika
mechi hiyo.Alikiri kuwa alihitaji kupiga penati.Lakini Super Mario alionesha
kujiamini na yeye akaweka imani kwa Mario kwani anahistoria kubwa katika kupiga
penati.
![]() |
Balotelli akifunga penati dhidi ya Beskitas |
Mario Balotelli ambaye kwa sasa yupo karibu sana na
mashabikiwa Liverpool katika mitandanao ya kijamii baada ya mechi
hiyo.Aliandika ujumbe wa kumshukuru Jordan Henderson ‘Hendo’ kwa kumwacha
akapige penati na kuwataka mashabiki wa Liverpool kuacha kuendeleza filamu ambayo
haina faida kwao.
Hili ni jambo dogo sana kwa Super Mario Balotelli tena hata
faini hajapigwa.Wakati akiwa Manchester city aliwahi kuvunja sheria aliyoweka
kocha wa wakati huo Robert Mancini ya kutomruhusu mchezaji yeyote kwenda
mjini kujirusha masaa 48 kabla ya mechi.
Mario Balotelli akiwa na rafiki zake walijumuika katika klabu
ya usiku na akapigwa faini ya dola 400,000.Na wala hakuwaza kama tatizo katika ubongo wake aliona ni jambo
dogo katika ulimwengu wake.
Yeye aliweka hadharani vile ambavyo wengine walificha na wala
hakuona tatizo.Februari 12 alipofunga goli alionesha fulana lililoandikwa
nakupenda Raffaela .Huyu ni msichana maarufu huku nchini Italia ni mwanamitindo
na anakashifa mbaya ya kushiriki katika sherehe za Bunga Bunga ambazo Silvio
Berluscon huziandaa kwa siri.
![]() |
Balotelli akimpa ujumbe mpenzi wake Raffaela |
Unakumbuka kituko chake cha mwaka 2012 aliposimama katika
shule moja mtaani huko Uingereza na kwenda kujisadia katika vyoo vya
wanafunzi.Bila kujali jina lake baada ya kumaliza haja zake akiwa na rafiki
zaake aliwasha gari lake la Bentley na kutokomea.
Ni binadamu aliyekuwa akiwaza tofauti na wengine kabisa alipokuwa
katika klabu ya Manchester City.Alipigwa faini ya dola 100,000 baada ya kukutwa
akicheza mchezo wa kurusha vishale(darts) na timu ya vijana wadogo.Alipoulizwa
sababu ya kufanya hivyo alisema alihisi upweke.
Ni mwafrika mwenye jeuri na rangi yake anajua anafuatwa na
vyombo vya habari kila anapokanyaga.Alitengenza habari kubwa april 2011
alipompa kijana asiye na kazi dola 1000 baada ya kushinda mchezo wa kamari dola
250000 katika Casino.
Ana ushawishi mkubwa katika upande wa michezo ya video(video
game) kwa kikatuni kinachojulikana na jina la Super Mario kimeonekana katika
game 200.Na ameuza zaid ya millionI 193 ya michezo ambayo yeye yumo.Jina ake limepelekea hili jina la Super Mario kuwa na ushawishi mkubwa
0 maoni:
Chapisha Maoni