KLABU YA SOKA YA  YANGA YA DAR ES SALAAM NA MAJI MAJI YA SONGEA ZIMECHUANA VIKALI KATIKA UWANJA WA MAJIMAJI MJINI SONGEA AMBAPO TIMU YA YANGA IMEIBUKA NA USHINDI WA BAO  MOJA KWA SIFURI.

BAO HILO LA YANGA LIMEFUNGWA KATIKA DAKIKA YA  KUMI NA TATU NA DEUS KASEKE BAADA YA MABEKI WA MAJI MAJI KUSHINDWA KUMZUIA HADI KIPINDI CHA  KWANZA KINAMALIZIKA YANGA ILIENDA MAPUMZIKONI IKIONGOZA KWA BAO HILO MOJA.


KATIKA KIPINDI CHA PILI TIMU HIZO ZILISHAMBULIANA KWA ZAMU HUKU MAJI MAJI IKIKOSA BAO LA WAZI KATIKA DAKIKA YA  36 KIPINDI CHA PILI AMBAPO ULINZI MKALI ULIKUWA UMEIMARISHWA KATIKA UWANJA WA MAJI MAJI HUKU TIMU YA YANGA IKIGOMA KUINGIA  KWENYE VYUMBA VYA  KUPUMZIKIA NA KUINGIA UWANJANI WAKITOKEA KWENYE GARI LAO.


0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top