Na hosea Mchopa
Mchezaji hatari wa klabu ya Chelsea Eden Hazard amekubali kuongeza mkataba wa miaka mitano kukipiga katika klabu ya Chelsea inayoshiriki ligi kuu nchini Uingereza.

‘Tangu nimekuja hapa mwaka 2012,Kila mara nimekuwa vizuri na klabu imekuwa ikinipa mchango mkubwa kwangu’alisema Eden Hazard


Mkataba huu utamfanya Eden Hazard mwenye miaka 24 kukaa darajani hadi mwaka 2020.Na kuweza kudhihirisha uwezo wake katika ligi kuu ya uingereza.

‘Ni kijana mdogo na anaweza kuwa mchezaji bora’Kauli ya kocha wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho
Mkataba wa Eden Hazard ambaye anaingiza karibu pauni 200,000 kwa wiki utagharimu  pauni milioni 57.

Mafanikio yake
Hizi ndizo idadi ya mechi na magoli ya Eden Hazard ambaye wataalamu wa soka wanamtabiria kuja kuishika dunia ya soka miaka ijayo.
Katika klabu ya Lille OSC mechi 194 magoli 50
Klabu ya Chelsea mechi 147 magoli  44

Mataji Ligue 1 mwaka 2010-2011
Couple de France 2010-2011

UEFA Europa ligi 2012-2013

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top