Na.Hosea Mchopa
Unataka mkataba mnono,unataka kupandishiwa mshahara katika
soka hakuna binadamu mwingine wa kumtafuta zaidi ya Jorge Paulo Agostinho
Mendes.Ana nguvu ya ushawishi katika ulimwengu wa soka.
Sasa yuko makini na Manchester united wakiangalia maslahi
mapya ya mteja wake David De gea.Wakipindisha maneno hataona tabu kuhamishia
meza yake Santiago Bernabeu kuitikisa duniani ya soka.
Majibu yake mafupi yaliyojijitosheleza hudhihirisha jinsi gani
analinda na kuwasimamia wateja wake .Ana jicho la Tatu kuweza kuona thamani ya
mchezaji kirahisi kuliko kawaida.
Jose Mourinho ilimpasa kumbwaga wakala wake Jorge Baidek na
kusaini kwa Mendes ambapo mwaka 20004 akajiunga na Chelsea.Jorge Mendes
akisimamia mpango mzima wa uhamisho huo.
‘Bila mjadala Jorge Mendes ni wakala bora kuwahi kufanya nae
kazi, ,Aliwajibika na anatenda haki kwa klabu’.Kocha wa zamani wa klabu ya
Manchester united Sir Alex Ferguson alinukuliwa akimpongeza wakala Mendes
ambaye alisimamia mpango wa Ronaldo kuhamia Real Madrid na kuvunja rekodi ya
usajili.
Jorge Mendes katikakati akiwa na wateja wake Josse Mourinho kulia na Christiano Ronaldo
Mawakala wetu watatu nchini Tanzania ambao wanatambulika na
FIFA John Ndumbaro,Ali Salehe na Mehdi Remtulla wanahitaji kumtazama
Mendes.Utashindwajwe kumtia Mkude mikononi ukamuuza Afrika ya kusini wakati
Mendes alimuuza Bebe Manchester united bila Alex Ferguson kumuona.
Mendes hucheza na akili za watu katika biashara anajua ujanja
wa bashara katika soka .Bebe kutoka mikono ya wakala wake Goncalo Reis hadi kwa
Mendes.Na kumfanya Mendes kuweka kibindoni paun milioni 3.6 katika uhamisho
wake kutoka Vicktoria Guimaraes kwenda United kwa ada ya uhamisho pauni milioni
9.
Ukiwataja mawakala hodari 12 wa michezo yote duniani
waliofanya mikataba ya minono .Hapa itakupasa
kumsahau kabisa Jorge Mendes na kumtaja Scot Boras.Boras mtaalamu ambaye
amesomea mambo ya mikataba na sheria katika chuo cha Mc George.
Dunia inamkumbuka Boars
mwaka 2007 kwa kusimamia mpango
wa uhamisho dola milioni 275 kwa mkataba wa miaka 10 wa Alex Rodriguez ‘A Road’ wa timu ya baseball ya New York
Yankee ya ligi kuu ya Baseball nchini Marekani.
Boras biashara zake nne kubwa katika ulimwengu wa
baseball amefikisha dola million 701 na
kuitikisa dunia ya michezo.Kumbuka alivyosimamia mauzo ya Alex Rodriguez dola
milioni 275,Max Teixeteira dola million 180,Bary Zito dola million 126 na Mat Holliday dola million 120.
Lakini ulimwengu wa Soka pamoja na uwepo wa mawakala hatari
kama Mino Raiola,Jonathan Barnet aliyepiga biashara kubwa ya uhamisho wa Gareth
Bale.
Mtaalamu wa dirisha la usajili Jorge Mendes anatawala kwa
kuwa na uwajibikaji kwa mchezaji wake hadi kufikia hatua Cristiano Ronaldo
alimwita ni wakala muwazi na mwenye haki.
Jorge Mendes toka kuwa dj na kumiliki klabu ya usiku mpaka
kuwaza kulishika soka kwa kuanza kufanya biashara yake ya kwanza ya mchezaji wa
kireno Nuno kutoka Victor de Guimaracia kwenda Deportivo la Coruna mwaka 1996.
Kutoka biashara ya kwanza nono kimataifa katika kazi yake ya
uwakala wa soka kwa kuuza Hugo Viana
kutoka Sporting CP kwenda Newcastle united kwa ada ya euro million 12.
Mpaka kuitikisa duniani kwa kufanya biashara ya kumuuza
Cristiano Ronaldo kwenda Real Madrid kwa ada ya euro million 80 huku
ikiripotiwa Mendes akiweka kibindoni euro million 4.Jorge Mendes anaiendesha
dunia ya soka kwa kufanya biashara zenye kuvutia na kucheza na tarehe za mwisho
wa dirisha la usajili.
Kwa mwaka 2014 katika usajili ameingiza paun million
30.Amefanya biashara ya James Ridriguez kutoka Monaco kwenda Atletico Madrid
kwa ada ya paun million 63,Angel Di Maria kutoka Real Madrid kwenda Manchester
united kwa ada ya pauni million 60.
Mendes pia alifanya biasahara ya kumtoa Diego Costa kutoka
Atletico Madrid kwenda Chelsea kwa ada ya pauni million 32 na Eliaquam Mangala
kutoka Fc Porto kwenda Manchester City kwa pauni million 32.
Kuna watu wanawasaini mkataba na wachezaji na wanasubiri
Jorge Mendes kuwaonyesha kwa watu na kuwapeleka kwenye klabu kuwa.Anaweza
kufanya chochote sasa mwaka 2012 nusu ya kikosi cha timu ya taifa ya ureno
kilikuwa na wateja wake.
Diego Costa,Yacine Brahim,Jose Mourinho,Luiz Felipe
Scorali,Carlos Quieroz,Simao Sabrossa,Anderson,Fabio Coentrao,Pepe,Angel di
Maria,Cristiano Ronaldo,Radamel Falcao,Ricardo Cavarliho,,Luis Nanni,Ricardo
Quaresmaa,Joao Moutinho,James Rodriguez,David de gea na Victor Valdes ni moja
ya watu wanaopata huduma ya Jorge Mendes.c
0 maoni:
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.