Toleo la 1

Na Hosea Mchopa #UO 1

Katika ardhi ambayo inafanya historia ya Tanzania kuwa tamu na ya kipekee duniani kwa kuwa na mto uliotengenesha na nchi ya Msumbiji.Ardhi iliyoleta jina la majimaji katika ulimwengu wa historia ya vita vya kugombania uhuru katika nchi ya Tanganyika.

Nikikutana na binadamu wacheshi wenye rangi kama yangu nyeusi kwa pamoja tukiwakilisha rangi nyeusi ya bendera yetu.Nikakutana na wamatengo,wayao,wandendeule,wabena,wangoni,wamakua na wandegereko.

Ama kweli Afrika ni asili tamu kuwahi kuifahamu.Ardhi ambayo inakubwa wa kilomita 63,498 na wakazi  1,117,166 kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2002.Majumba ya asili ya kizamani inafanya ujue ni afrika huku maduka mengi yakijihusisha na uuzaji wa madini.Kuthibitisha neema ya mungu ya kuijaza Afrika vitu vya thamani.

Huu ni mkoa wa Ruvuma wenye wilaya sita ulionipa siri ambayo ni dhahabu serikali ya Ruvuma inahitajika kuitafiti zaidi.Nikitokea moja kwa moja katika moja ya mikoa midogo Tanzania mtwara wenye kilomita 16,720.

Urefu wa safari haukuwa ni tatizo kwangu nilihitaji kujifunza mambo mengi mapya maisha mwangu nikiwa nina sura nyingine.Sura ya kuiandika nchi yangu Tanzania popote pale nitakapokanyaga kwani naamini tumebarikiwa vingi.

Mwenye Mpelia Kamtande katika kijiji cha Mtonya aliweza kuingia katika historia yangu kwa kunipa siri ya  mlima Chamanga ambao ni rahisi kuonekana na kuufikia ukiwa katika kijiji cha Mtonya.

Nikifuatana na mwenyekiti wa kijiji na watu wa karibu wa kijijini nilipelekwa moja kwa moja kwa mzee Mwenye mpelia.Yeye alinipa utofauti mkubwa uliopo kati ya mlima wa Chamanga na milima mingine ninayoiona.

Mlima huu una maajabu ambayo yakiangaliwa na serikali unaweza ukawa chanzo cha mapato kwa wanakijiji ambao wanategemea kilimo pekee.Kwani watafiti wakijulishwa vyema uwepo wake wanaweza wakagundua vingi vilivyomo ambavyo vinaweza kuwa vivutio vya utalii.

“Mlima huu,bwawa lake,na uwanja mkubwa uliomo ndani aliyefanywa watu wajue kuna nini.Ni marehemu Jua kali mwela ambaye kazi zake ni kuwinda Nungunungu.Na kukuta maajabu ya ya uwanja mkubwa amabao unaweza ukakusanya kijiji cha Mtonya”.

Ndani ya pango hilo kabla ya kuingia lazima upitie mbepesi kwenye msola(mti) ambao unafagiliwa ili kumfanya Nyoka mkubwa anayeishi katika pango ile aingie katika Chungu cha maajabu.Chungu ambacho mpaka leo hakuna aliyethubutu kukisogelea na kujua kina nini zaidi.

Watu wanaofanya hivyo mara nyingi ni wale waganga ambao hutumia maji haya mpaka kesho kuwatibu watu wenye mashetani na majini.

Maajabu yanayoweza kuleta tija ni uwepo wa eneo kubwa ambalo ndani yake kuna wanyama kama Simba na chui wanaozaliana na kuishi humo.Bila mnyama Nungunungu kuweza kuingia katika kitundu Jua kali asingeweza kugundua chochote.


ITAENDELEA ………..JUA SAFARI  MPAKA MALIASILI NA YALIYOMO ZAIDI KATIKA MLIMA CHAMANGA

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top