Na Hosea Mchopa #UO 1

Dunia imegawanyika vipande vipande kinachosubiriwa na kusagwa sagwa na kupoteza kila kilichomo.Hii ni hatari ambayo haiwezi kuzuilika kama ilivyo kwa kifo.Lakini umewahi kuwaza kuwa unaweza ukawa kijana mpaka kifo chako.Haijalishi utakufa na miaka mingapi.

Mimi ninawaza sawa kama Henry Ford mmliki wa kampuni ya Ford Motor na mwandishi wa kitabu cha My life and work kwa hili.Mtu yeyote anayeacha kujifunza huyu ni mzee hata kama ana miaka 20 au 15.Na yule anayejifunza huyo ni kijana.Na siku zote weka akilini kuwa u kijana na unaendelea kujifunza.

Katika jamii niliyopo nageuka kulia na kushoto na kutana na vijana wanaopenda vitu vilaini wakiamini wanahitaji akili ipoe kwa manufaa ya baadaye.Hawapendi kujifunza,wanapenda kufanya wanavyohisi bila utafiti wowote uwe wa mahandishi au sauti.

Ukiwa kijana unakuwa unajiamini,wakati mzee huwa mwoga kwa kuwa u hafifu.Ukiwa kijana unakuwa na matumaini wakati ukiwa mzee unakuwa hauna unachotumaini.Hii ndo siri kwa nini vijana wengi Tanzania hawajiamini na hawana matumaini.Wao wamezeeka kwa kuwa hawapendi kujifunza.

Kujifunza ni zaidi ya kusikiliza radio na kuweka kichwani ni kutafiti zaidi,kuchambua kitu kiundani.Leo hii hili ni kosa la jinai kwa kijana anayeishi kwa kujifunza huonekana anajizeesha.Wao wanachukia uzee wakati kutojifunza ni uzee tosha.

Napata shida sana moyoni nikisikia Taifa linategemea kitu kutoka kwetu eti tuje kuokoa kizazi kijacho.Tumerahisishiwa ufaulu wa kidato cha nne,tunarahisishiwa ufaulu katika vyuo vyetu tunapita kirahisi.

Tunapoteza muda kuwaza kwa nini wazee wa zamani walikuwa na uwelewa mkubwa.Wao ilikupasa uwe unafahamu kitu kiundani ndipo upate heshima katika jamii ya kitanzania.Sisi leo hii cheti na makaratasi yaliyotengenezwa huleta uimara wa mtu kulikoni kile alichonacho.

Henry Ford aliyezaliwa mwaka 1863 mwezi julai 30 na kufariki april 7 mwaka 1947.Akiwa na miaka 26 alikuwa tayari amesoma tafiti mbalimbali zilizomuwesha kuwa na afya ya akili.Hii ilimpelekea kuwaza kutengeneza gari lake la kwanza likijulikana kama quadricycle mwaka 1896.

Ili uweze kuwaza kwa kina na kuvumbua mambo mapya hautajiki kuwa msikilizaji na mpokeaji tu.Lazima upende kusoma kiundani ukitengeneza ndoto pevu zilijengeka katika mbinu za kisomi na kuwa na mlango unaoshangaza.

Leo hii vijana ni wepesi wa kusahahu hata ahadi walizoahidiwa na viongozi wao,miaka mitano ikifika wakiahidiwa hushangilia tena.Akili zao zimezeeka kwa kuchukia watu wanaobuni na kuwaza miaka miatano ijayo wakati wao kesho hawaijui.

Vijana wanatumiwa na wazee katika upande wa siasa bila kujua huku wakilalamika bila kukoma juu ya ugumu wa maisha.Akili zao hazina afya tena,wamekosa uwezo wa kutafakari mambo kwa jicho la tatu.

Wamechukuliwa na teknolojia upande hasi,si chanya kama inavyopaswa kutumiwa kusambaza hata maneno ya mungu.Wao imewafanya washindwe kabisa kutembelea hata nyumba za ibada.Hii ni siri kwa nini busara na unyenyekevu huishi mbali nao.

Mahatma Gandhi  Bapu mwanaharakati wa india huru alisema ishi kama utakufa kesho.jifunze kama utaishi milele.Asingejifunza angeutumiaje ujana wake kuokoa jamii yake.Leo hii vijana ndio wanaotumiwa na wanasiasa kuharibu maendeleo kuja kuwashangilia wanapoahadaa wananchi.

Elimu si kujifunza dondoo na takwimu bali ni kukiweka kitu kichwani kukifuatilia na kukitumia maishani.Kutoka hapo ulipo umefungwa na uvivu wa kujifunza,kukata tama kunakotokana na kushindwa kujua wengine walifanyaje.

Wazee wote wanaondelea kushangaza dunia walijifunza mengi katika muda wetu.Marie von Ebner Eschenbach mwandishi wa Austria aliyezaliwa nchi ya jamhuri ya Czech na mwandishi wa vitabu vya Their Pavel, Beyond atonement alisema katika ujana tunajifunza kwa sababu ni umri tunaoelewa.Usipotumia huu mda vyema utakuwa mzee mara mbili kimwili na kiakili.

Vijana wengi wa Tanzania ukitukuta katika makundi yetu tunasikistisha,tumekosa ubunifu kabisa na akili zetu zimezidi kulala maradufu.Tunasema tuliyoambiwa bila ya kuyatafiti,tukiulizwa tunaishia kuimba wimbo wetu alisema.

Bado nipo chuoni najifunza na nawasoma vijana ambao hawajui hata fani yao wanaoisomea nini kinaendeea katika serikali kuhusu wao.Vijana ambao watakuja kupiga kura ya kumchagua rais wa Tanzania kwa kipimo cha anavyotangazwa katika vyombo vya habari na sio sera zake.


Si rahisi kuhisi umri umesogea kama akili yako inafanya kazi kama kijana.Umri ni kuamua moyoni ila usipoamua uanabaki vilevile.Amini unaweza ukaishi milele kijana ukiamua kutuamia ujana wako kujifunza.Ukiwa mzee wa mwili pekee utafurahi kufunua kinywa ukiwa umezungukwa na vijana wengi wakichukua yaliyomo moyoni na kujifunza.Jifunze zaidi uipeleke Tanzania mbali zaidi..Ujana ni kujifunza na kubadilisha.
18 Mar 2015

0 maoni:

Chapisha Maoni

:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top