Na Hosea Mchopa #UO 1
Huko nchini marekani JACKSONVILLE
FLORIDA wanadoa Tito na Amanda Watts wamekamatwa na polisi kwa kosa la kuuza
tiketi feki za dhahabu za kuwazesha watu kwenda mbinguni.
Baada ya kukamatwa Tito Watts
akiongea kwa kujiamini alisema
‘’Sibabaishwi na walichokisema
polisi.Hizi ni Tiketi za dhahabu halisi na sio kweli kuwa nimepulizia rangi.Ni
Yesu mwenyewe ndiye alinipa pale nyuma ya mghahawa wa KFC huku akiniambia
nikauze ili nipate fedha za kwenda anga ya juu’’Tito Witts alisema
‘’Kwanza nilikutana na kiumbe wa
ajabu wa sayari nyingine anayeitwa Stevie ambaye aliniambia kuwa kama nikiwa na
fedha ataninyakua mimi na mke wangu kwenye ungo wake unaopaa mpaka kwenye
sayari yake amabayo imeumbwa kwa cocaine tupu.Nitaweza kuvuta unga wa cocaine
kadri nipendavyo,tena bila malipo.’’
Tiketi ambazo iliwagharimu watu
waliomini kutoa dola 99.99 ili kupata tiketi moja ya kuweza kufunguliwa lango
la mbinguni.
Kosa kubwa ni kuwa Tito aliwaambia
watu kuwa zilitengenezwa kwa dhahabu tupu na ukifika langoni mbinguni
ukionyesha tu unaruhusiwa kupita.
Polisi wao wanakana na kusema
wamemakamata kwa kosa la kulaghai kwa kudanganya ni dhahabu tupu wakati ni miti
tu ambayo imepuliziwa rangi ya dhahabu.
Kwa upande wa polisi kuuza tiketi
za kwenda mbinguni sio kosa ,kosa ni kulaghai watu juu ya tiketi za dhahabu
tupu.
Tito akiongea kwa kujiamini
alisema wajaribu kumpeleka mtu asiye na
hatia jela ndio watakiona cha mtema kuni.Kama ni kukamata basi akamatwe YESU kwa sababu yeye ndio aliyenipa tiketi
hizi na kuniambia nizue.
Na akahidi kuwa yuko tayari kumrekodi Yesu kwa kificho ili watu wanaombeza waamini juu anachosema
.
Watu hao wamekamatwa na jumla ya
dola 10000,mabomba matano ya kuvutia unga na mamba mdogo
Kwa upande wa mke Amanda amesema
nia yao ilikuwa kuondokana na dunia hii tuende zetu anga za juu tukavute unga
wa cocaine.
‘Sijafanya chochote.Mume wangu
ndio alikuwa anauza hizo tiketi za
dhahbu za kwenda mbinguni.Mimi nilikuwa muangaliaji’alisema Amanda
0 maoni:
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.