#news room 


Rais wa UKRAINE Petro Poroshenko( mbele) akiondoka baada ya mazungumzo ya kusaka amani mashariki mwa Ukraine.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linataraji kukutana kwa dharura leo Jumapili ili kuweka mikakati ya kuimarisha makubaliano ya kusitisha mapigano Mashariki mwa Ukraine yaliyofikiwa mjini Minsk nchini Belarus, wanadiplomasia wamesema.
Wajumbe 15 wa baraza hilo wanajiandaa kupitisha mapendekezo yaliyoandaliwa na Urusi yanayotoa wito kwa pande zote kutekeleza makubaliano hayo ambayo yanatoa makataa ya kusitisha vita kuanzia kesho Jumapili.
Makubaliano yaliyofikiwa na rais wa Urusi Vladimir Putin na viongozi wa Ukraine , Ufaransa na Ujerumani, yameonekana kushindwa huku mapigano makali ya siku Ijumaa yakisababisha vifo vya watu 28.

14 Feb 2015

0 maoni:

Chapisha Maoni

:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top