Kufikiri vyema kwa
ajili ya baadaye kunahitaji kujitambua kuwa maisha yako ya leo yaliandaliwa na
waliopita.Haupaswi hata dakika moja katika maisha yako kujifikiria wewe peke
yako.Tafsri ya maisha yako itakuwa fupi sana u mbinafsi.
Sasa tujiulize
utawekaje ubinafsi katika jambo ambalo linagusa zaidi ya watu milioni 40 tena
litawaendesha kwa miaka 5.Hii ni safari ambayo bado watanzania wamejiandaa
kukata tama kwa kuamini hawana uwezo wowote wa kuamua matokeo.
Si mbali ni karibu
kuweza kuamini ukiwaza kwa ajili ya kizazi kijacho,ukiweza kuwaza hivyo unaweza
ukagusa sehemu usiyoitarajia.Unafahamu hamasa unayopata ukipanga jambo jipya
lenye kugusa maisha yako.Ndivyo amini unavyoweza kubadilisha malalamiko yako ya
miaka mingi iliyopita.
Nakumbuka Agosti 28
mwaka 1963 katika kumbukumbu ya Lincoln,Washington DC Martin Luther alipoonyesha
maana halisi ya binadamu anayetambua uwepo wake duniani.Aliweza kuwaonyesha
watu kuwa kuwaza kwa kina kuhusu kesho kunaweza kukakufanya uamini kila kitu
kinawezekana.
![]() |
Martin Luther akihutubia tarehe 28 agosti 1963 |
Martin Luther aliamini
vitu ambayo watanzania waliokuwa na mioyo iliyolala wasingeweza hata kuvumilia
kumsikiliza.Sisi tunaishi na roho za bora hili kuliko lile lijalo,huku woga
ukiwa katika kila sentesi itokayo vinywani mwetu.
Woga ni mbaya huharibu
kabisa nafasi ya kitu halisi ambacho kinaamua mafanikio yako maishani.Chaguo
ndio kitu muhimu katika mafanikio ya kitu chochote duniani.Kila kitu
unachokichagua lazima kiwe na umuhimu kwa kizazi kilichopo na baadaye.
Usiogope kuwaza kuwa
unataka kuiona Tanzania inayoongoza kwa elimu katika umoja wa jumuiya wa nchi za Afika
Mashariki baada ya miaka 5.Chaguo lako ndio litachagua mwelekeo wako wa nini
unastahili kutokana na ulichokiwaza kiwe.Hutakiwi kabisa kuficha maono yako
nyuma ya pazia na kutanguliza roho ya woga kuwa mabadiliko katika ardhi yetu
hupangwa na watu wenye nguvu.
Tunaelekea katika
uchaguzi mkuu wa wa nchi ya Tanzania ambayo ina sifa ya amani na upendo.Lakini
wote tuishio tunajua nini kipo katika ardhi hii,tunafahamu mambo ya kushangaza
ambayo yanazaliwa na kuachiwa bila hatua kuchukuliwa.
2015 ni wakati wa
kuwaza katika maono ya mbali na kuweka woga wetu pembeni ambao umeingia katika
roho zetu.Woga ninaongelea ni ule wa kuamini mimi siwezi kubadili Tanzania kwa
kura yangu,kwa mawazo yangu,kwa uwepo wangu katika sehemu yoyote ile.
Woga hupelekea mtu kushindwa
kutafsri vyema mambo yatakiwavyo kuwa.Woga humfanya mtu kushindwa kutofautisha vitu
vidogo ambavyo yeye anahitajika kuvipata.Humfanya mtu kuamini hawezi kuileta A
kama aliye juu anapenda B.
Lazima ujue Tanzania
ya leo na ijayo watu wanahitaji Kiongozi ambaye anaishi kwa tafsri halisi ya
uongozi.Mtu ambaye yupo katika nafsi ya urais,ubunge kufanya majukumu ambayo kiongozi wa nafasi
hiyo anapaswa kufanya akifuata sheria na kanuni zilizowekwa ili aweze kuongoza
kundi kubwa la watanzania.
Tutofautishe kabisa na
madikteta ambao wanasimama katika nafasi ya urais kama makocha wanaotaka kila kitu
ambacho wao wanachopendaa timu ikifanye.Wale ambao hawahitaji michango zaidi ya
kuelekeza watu wafanye wao wanavyopenda bila kufuata kanuni.Na wanafanya hayo
yote kwa kauli kuu kuwa wa ndio wenye mamlaka.
Woga utamfanya mwanao
ajae akute serikali iliyokosa uwazi kwa kuwa uliuendekeza ukashindwa kuamua
chaguo sahihi.Ukashindwa kumchagua kiongozi ambaye anafanya kitu inavyopaswa
hata kama hakuna mtu anayemtazama na kumsifu.
Kama utaweka woga
mbele utashangaa kuona kiongozi sahihi akiwaza kuiona Tanzania ikiwa ina umeme
na maji vijijini.Hivyo utaishia kuiletea Tanzania kiongozi mwenye maono na
kuifanya familia yetu ibakie vilevile kimaendeleo.Na siku zote kiongozi asiye
na maono huwa hajitambui kuwa yupo katika uongozi kama wajibu tu anapaswa aache
alama akitoka.
Tunahitaji kusikilizwa
watanzania kwani kuna vitu vingi vitahitaji marekebisho ambayo yataleta faida
katika nchi yetu.Tutampata wapi kiongozi anayetusikiliza kama woga wako
umekupeleka kushindwa kumtofautisha kiongozi anayekujali wakati wa kampeni na
kiongozi ambaye anajali shida za watanzania?.
Kiongozi ambaye
atakuwa ana uwezo wa kusoma alama za nyakati na kutoogopa kufanya maamuzi
ambayo yanaweza hata yakamuumiza yeye kwa ajili ya usalama wa watanzania.
Martin Luther aliamini
maisha watoto wake siku moja watakuja kuishi katika taifa la Marekani ambalo
hawataishi kwa kuangaliwa rangi zao za ngozi kama ilivyokuwa wakati huo.Aliacha
woga akamini pamoja na wabaguzi wana nguvu lakini jamii ikiamua kutaka kilicho
bora inawezekana.
Jenga daraja jipya kuelekea
2015 katika moyo wako ukiishi kwa maono na kutumia nafasi ya chaguo vyema kwa
ajili ya Taifa.Ishi kwa ndoto!.
0 maoni:
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.