Na Hosea Mchopa #UO 1

Mchezaji haruhusiwi kwenda mjini kujiburudisha masaa 48 kabla ya mchezo.Hii ndio ilikuwa kanuni ya kocha wa zamani wa Mancheser City Robert Mancini.Na Mario Balotelli aliwahi kuadhibiwa kutokana kukiuka kanuni hii.

#hii kwa ajili yako


Inawezekana kukawa na hali inayoashiria Luis Enrique na Lionel Messi bado hawajawa katika muungano unaohitajika.

Leo  asubuhi ikiwa ni masaa 48 kabla ya kuelekea katika mchezo mkali wa ligi ya mabingwa ulaya kati ya Barcelona wakialikwa na Manchester  City katika dimba la Etihad.

Lionel Messi,Gerard Pique na Cesc Fabregas mchezaji wa Chelesea walikuwa wakijumuika pamoja katika Casino .
Lionel Messi,Fabregas na Luis Enrique wakiwa nje ya Casino

Akizungumza Katika mkutano na wahandishi wa habari za michezo kuelekea mchezo wa UEFA.Kocha Enrique ameonesha wazi kutohitaji kulizungumzia suala hilo kwa sasa.

Ni maisha yangu binafsi.Ni kauli ya Gerard Pique akijibu kashfa ya kwenda kwenye  Casino  masaa 48 kablya ya mechi.Huku kocha wake Enrique akihitaji kutoulizwa maswali yasiyohusu mpira wa miguu na hatovutiwa kuyajibu yale yaliyo nje ya kazi yake.

Uhusiano mbovu kati ya kocha Jose Enrique na Lionel Messi yalipamba moto pale kocha alipoamua kumweka benchi Messi wakati timu yake ikipewa kichapo cha goli1-0 na Real Sociedad.
Gerard Pique na Lionel Messi wakiwa mazoezini


Bado Enrique ameweka wazi kuwa mahusiano na wachezaji wake yako sawa na anapenda kuongelea na kuchambua kuhusu vitu vinavyohusu mpira wa miguu na sio maisha binafsi.

Lakini jamii na familia ya soka tunamtambua na kumfahamu Enrique kuwa ni baba wa nidhamu.Na ni kitendo kisichopenedeza kwenda klabu masaa 48 kwenda klabu kabla ya mchezo.Je ataamua nini siku za usoni.
Kocha wa klabu ya Barcelona Luis Enrique akizungumza na wahandishi wa habari hii leo


Enrique alipotua Stadio Olimpico Roma alifanya maajbu makubwa sana ya kupambana na wafalme waliotengenezwa miaka mingi katika klabu hiyo.Daniel De Rossi pamoja na Fransico Totti walipambana na roho ya udikteta wa nidhamu wa Enrique.


Hakuweza kuvumilia kuona Danie De rossi anachelewa katika mechi ya maandalizi kwa sababu ni mkongwe wa timu.Hakuwa na mashaka kumwacha nje nahodha wa timu Totti baada ya kuvunja sheria zake za kutofanya mazoezi ipasavyo kabla ya mechi.
24 Feb 2015

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top