Na Hosea Mchopa #UO 1
Ni dhahabu nyeusi
kutoka Lagny sur Marne “Polpo Paul II’ au Patric Viera mpya.Wataalamu wa soka
wanamtambua kwa vielelezo vitatu nguvu,ujuzi na ubunifu.
Ukiwa Italia ukiperuzi
kona zote za michezo La Repubblica ,II Messaggero na La Gazzeta Dello Sport
lazima ukutane na sura yake.Kocha Alex Ferguson kila mara hukubali kumwacha
binadamu huyu alifanya makosa makubwa sana.
Mchezaji wa kimataifa
wa Hispania na Manchester united Juan Mata anakata tamaa kila akiona jina la
Polpo Paul II limeambatanishwa na Manchester united.Anajua hivi sasa
ukizungumzia katikati mwa uwanja katika ulimwengu wa soka unamtaja yeye.Mata
anajua kibarua kimeota nyasi.
Dhahabu nyeusi Paul
Labile Pogba ‘Polpo Paul II’ mwenye kilo 80 ndiye anayetishia dunia ya soka
hivi sasa.Sekunde,dakika na masaa yanavyozidi kwenda akiwa katikati ya uwanja
ndivyo thamani ya pesa yake inavyoongezeka kwa kasi kwa vitu anavyovifanya.
Paul Pogba
Akiwa bado kijana mdogo
mwenye umri wa miaka 21 amefanya kila kitu ambacho mchezaji kamili anatakiwa
akifanye.Ama hakika amekamilika kiuchezaji,miguu mirefu na mwili imara
humtambulisha yeye ni nani.
Ukiitazama miguu yake
itakupa somo kuwa yuko tayri kukimbizana nawe na kukunyang’anya mpira vile
apendavyo.Patric Viera mpya anayemezewa mate na vilabu vikubwa barani ulaya.
Mkongwe wa Italia na
Juventus Andre Pirlo amemtaka aachne na
fikra za kuhamia igi kuu ya uingereza na kuamishia akili zote Juventus.Lakini
kwa hali hii ya kawaida nani ataweza kumzuia Pogba asiondoke Juventus.
Miaka 21 kila umri
unaposogea ndivyo anavyozidi kuimarika na kumfanya kocha mwenye matukio Jose
Mourinho kukuna kichwa akimtazama Abramovich.Ni kama mvinyo siku zinavyozidi
ndivyo huwa mtamu zaidi.
Mkongwe wa ufaransa na
mshambuliaji wa zamani wa Chelsea takribani miaka 4 Nicolas Anelka anahitaji
kumuona Paul Pogba anajiunga na klabu ya Chelsea anakuwa katika mikono ya
tajiri Roman Abramovich.
Anelka anahitaji
kumuona anaenda Real Madrid katika klabu kubwa duniani akajifunze mengi kutoka
kwa kocha mwenye rekodi ya kipekee kuchukua UEFA akiwa na AC Milan na Real
Madrid Carlo Anceloti.
Pogba mzaliwa wa Lagn
sur Mane ufaransa alitwaa mchezaji bora chini ya miaka 21 barani ulaya katika
tuzo za Golden Boy mwaka 2013.2014 akatangazwa kama mchezaji bora barani ulaya
chini ya miaka 23 katika tuzo za Bravo.
Mchezaji wa Juventus Paul Pogba akishangilia goli
Mwaka 2014 ulikuwa wa
kipekee kwake katika kombe la dunia aliweza kufunga bao kwa timu ya taifa
brazili tarehe 30 juni 2014.Katika mechi dhidi ya timu ya taifa ya
Nigeria.Kutokana na kiwango alichoonesha katika kombe la dunia 2014
akachaguliwa kuwa mchezaji bora mdogo wa dunia.
Kiungo mkabaji na
kiungo wa kati ni majukumu ambayo ukimpa hautajutia uamuzi wako kabisa. Ni roho
ya Juventus ana jeuri ya kufikisha
mipira atakako,ana uwezo wa kufika kila kona ya uwanja.
Mechi 19 za Seria A
amefunga mabao 6 na kutengeneza goli 2 katika dakika 1700 tu alizocheza.Dakika
537 kwa upande wa ligi ya mabingwa ulaya ameona nyavu mara 1 na pasi 1iliyozaa
goli
Ana uwezo mmkubwa wa
kunyang’anya mipira na kupiga pasi ndefu zianzofikia wahusika.Msimu huu ana
wastani wa silimia 83 wa kupiga pasi sahihi.Kazi ziliwashinda viungo wengi
waliopo kwa bahati kalbu kubwa.
Hakuna taarifa
inayovutia wapnzi wa soka kama taarifa ya Louis Van Gaal kusema anahitaji
kiungo mbunifu zaidi katika dirisha la usajili lijalo.Sasa Wayne Rooey Pekee
ndio anaweza kukabili majukumu hayo United.Hili ni fumbo tu lakini Van Gaal
anamuhitaji Pogba.
Macho ya vyombo vya habari hayana mashaka
kabisa juu ya mapungufu yaliyopo Manchester united yanahusiana kabisa na
uhitaji wa kiungo hatari kama Pogba.Je ? ni nani hasa atajiunga na Manchester
United,hatupaswi kusahau kuhusu IIkay Gundogan ambaye ananukia kinywani mwa Van
Gaal.
Paul Pogba akiwa katika jezi la Manchester united
0 maoni:
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.