Na hosea Mchopa #UO 1

Fc Basel ikiwa nyumbani St Jakob Park kuikaribisha Fc Porto katika usiku wa mabingwa ulaya mambo ya kuvutia yalijitokeza katika mechi hiyo ngumu ambayo iliisha kwa sare ya goli 1-1.
Kocha wa Fc Porto Julen Lopetegui na kocha wa Basel Paulo Sousa  


Mwamuzi Mark Clattenburg ambaye msimu uliopita alikosolewa vikali na kocha wa Juventus ,aliongoza mechi kali na ya kipekee mbele ya mashabiki 34,464 waliokata tiketi kutazama mechi hiyo.

Dakika ya 11 tu iliwapa raha mashabiki wa Fc Basel baada ya mchezaji wa kimataifa wa Paruguay Derlis Gonzalez kufunga bao na kuwapa matumaini Fc Basel katika mchezo huo.
Gonzalez wa Basel akifunga goli dakika ya 11

Clattenburg pamoja na kukata goli la Porto dakika ya 79 aliwazawadia penalty Porto na Danilo kukwamisha wavuni na kufanya matokeo yaishe kwa goli 1-1.
Danilo akifunga goli kwa njia ya penati 


MAMBO YA KUVUTIA
Katika mechi ya jana mwamuzi Mark Clattenburg alitoa kadi 9 za njano.kadi 5 kwa Basel na 4 kwa Porto.
Mwamuzi Clettenburg akimuonesha kadi ya njano mshambuliaji wa Porto Torres


Kadi hizi zimeweka rekodi na kuifanya kuwa mechi peke kuwa na kadi nyingi kwa masimu huu.

Fc Basel hawajawahi kuingia katika hatua ya robo fainali ya mashindano ya ulaya tangu msimu wa mwaka 1973-74.


Jana Danilo alikuwa ni mchezaji wa tatu wa Porto kufunga kwa njia ya penati msimu huu baada ya Ricardo Quaresma na Jackson Martnez kufanya hivyo.
Mchezaji wa klabu ya Porto Danilo





#UO TUNAAHIDI KUKUPA KILE UNACHOSTAHILI

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top