Na hosea Mchopa #UO 1
Usiku wa mabingwa ulaya ulizidi kushamiri kwa kuleta mambo ya
kuvutia na rekodi za kipekee katika usiku wa jana pale mabingwa Real Madrid walipokaribishwa na Schalke 04.
Pamoja na kumbukumbu mbaya za Schalke kutolewa na Madrid katika hatua kama hii kwa
jumla ya goli 9-2.Jana wakiwa nyumbani mbele ya mashabiki 54,442 walijitahidi kupambana vilivyo kuweza kuwazuia Madrid
wasifanye maajabu zaidi.
Ilimchukua dakika 26 mwamuzi Martin
Atknson kupuliza kipyenga cha goli baada ya mchezaji bora wa dunia Cristiano
Ronaldo kumaliza ukame wa mabao baada ya kutoona wavu kwa mechi tatu
zilizopita.Alikuwa ni Dan Carvjal ndiye aliyetengeneza mpira mzuri na Ronaldo
akiumaliza kwa kichwa.
Kama haitoshi Ronaldo
jana akageuza usiku wa mbingwa ulaya kuwa wake baada ya kutengenza goli la
pili kwa Marcelo ambaye aliweka kimiani goli dakika ya 79.
MAMBO YA KIPEKEE
KATIKA MECHI YA SCHALKE NA REAL MADRID.
Timu ya Schalke haijawahi kushinda kombe la mabingwa ulaya
lakini kocha wake pekee Roberto Di Matteo amewahi kulibeba kombe hilo akiwa
katika klabu ya Chelsea.
Kocha wa Schalke Di Matteo
Beki raia wa Brazil Marcelo goli lake la pili jana dakika ya
79 ndio goli lake la pili kwa msimu huu.
Marcelo akishangilia goli lake alilopachika dakika ya 79
Cristino Ronaldo Jana amefanya maajabu ya aina yake kwa
kufunga magoli 58 katika michezo 58 ya ligi ya mabingwa ulaya.
Mshambuliaji wa Real Madrid Ronaldo akishangilia goli lake la 58
Klabu ya Real Madrid imeitambia Bayern Munich baada ya
kushinda michezo 10 mfululizo bila kufungwa.
Vikosi vya jana
Schalke 04
· 40 Wellenreuther
· 22 Uchida
· 04 Höwedes
· 32 Matip
· 31 Nastasic
· 15 Aogo
· 12 Höger (Meyer - 80' )
· 33 Neustädter (Kirchhoff - 57' Booked )
· 09 Boateng
· 25 Huntelaar (Platte - 33' )
· 13 Choupo-Moting
Real Madrid
·
01 Casillas
·
15 Carvajal (Arbeloa
- 82' )
·
03 Pepe
·
02 Varane
·
12 Marcelo
·
16 Borges
·
08 Kroos
·
23 Isco (Illarramendi
- 85' )
·
11 Bale
·
09 Benzema (Hernández
- 78' )
·
07 Ronaldo
0 maoni:
Chapisha Maoni