Na Hosea Mchopa #UO 1
Ushindi wa jana wa Juventus dhidi
ya Dortmund umewafanya wafikishe mechi 47 bila kufungwa wakiwa katika uwanja wa
nyumbani.
#hii kwa ajili yako
Pamoja na klabu ya Borussia
Dortmund kutawala mchezo kwa asilimia 53 kwa 41 za Juventus walikubali kichapo
cha goli 2-1.
Kinara wa magoli wa Juventus
Carlos Tevez alitumia dakika 13 tu kuweza kumgalagaza kipa wa Dortmund
Weidenfeller.
Marco Reus kiungo anayevutia barani
ulaya kwa sasa alimtungua mkongwe wa Italia kipa Buffon dakika ya 18 tu na
kurejesha hali ya ushindi Dortmund
Alvaro Morata akafunga bao la pili
kwa Juventus dakika tatu kabla ya kipindi cha kwanza kuisha na kufanya wenyeji
watoke kifua mbele kwa jumla ya goli 2-1.
Kocha wa klabu ya Dortmund Jurgen
Klop moja kwa moja ameyakubali matokeo hayo kuwa yalikuwa ya haki na
kuwapongeza Juventus kwa kuweza kutumia vyema nafasi mbili kubwa walizopata.
Mechi za leo
0 maoni:
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.