Na hosea Mchopa
Nikikumbuka michano ya Profesa Jay kwa lugha ya Kiswahili akipanda
na kushuka kwa nidhamu ya muziki halisi.Akitamka neno kwa upekee ili ajenge
mtindo wake katika jamii.Ni binadamu gani angechoshwa na ladha zake kama
angefika katika anga za kimataifa kwa utamu wa lugha ya Kiswahili.
Yuko wapi Jay Mo akiziadhibu midundo ya P Funk ‘Majani’
hatujamsikia harakati katika muziki wa kimataifa.Leo hii hata Mwana FA huyu sio
kabisa mimi ninayemuhitaji akipambana na darasa kwenye chati za muziki wa
Nyumbani.AY pekee anafariji wakongwe sasa anauwezo hata wakutamka anataka
kufanya kazi na wasanii wa daraja la kwanza marekani.
Jay Mo na Mchizi Mox
Dapo Oyebanjo D Banj leo
hii ana uwezo wa kusimama mbele ya dunia na kujitapa kuwa ameishi katika
kiwanda cha muziki kwa miaka 10 na anajivunia kwa alichokifanya.Amefanya muziki
katika hadhi ya chini Nigeria na kufikia anga za kimataifa.
Ana mafanikio makubwa ni moja wasanii 20 Afrika wenye pesa
ndefu na wenye ushawishi mkubwa.Safari yake hawezi kuisumulia peke yake wengi
tumemuona alivyojitahidi kupigana katika
anga za kimataifa.Leo hii Lady Jay Dee,Afande Sele,Juma Nature wasanii ambao
wamefanya muziki kwa muongo mmoja wanatamani kufika hapa.Lakini leo bado ni
wasanii wachanga katika anga za kimataifa.
Mdau wa Bongo Fleva kutoka chuo kikuu cha Jordan Morogoro
Michael Dachi ambaye naye ni msanii wa bongo fleva.Anasema inaumiza wasanii wengi
wa zamani ambao ndio walikuwa na ladha za kipekee zenye uasilia wa Bongo Fleva
wengi hawana cha kujivunia nje ya mipaka yetu.Msanii gani wa Nijeria angeweza
kusimama na kupambana na ladha za Juma Nature kama angekuwa yupo kimataifa.
‘Kibao changu cha
kwanza kilitoka mwaka 2004.Albamu yangu ya kwanza niliitoa mwaka 2005 na kila
mara nilisema nilikuwa mburudishaji na niliomba kuwa nitakuwa msanii mkubwa
kutoka nje ya afrika.Nitakuwa mfanyabiashara ,unaajua kila mara nina ndoto
tofauti’.Dbanj akieleza historia yake ya muziki.
Hapa Dbanj ananionesha jinsi gani yeye hakuta kuwa kinara wa
Lagos pekee hayakuwa malengo yake makubwa.Yeye alikuwa anawaza kuja kuwa kinara
katika muziki wa Afrika tena huku unia ikimshuhudia.Wasanii wetu wengi wao
wanatosheka wakiiteka mikoa 26.wakiskika Kenya wanaona tayari wao ni wa
kimataifa.
Ninapohesabu baraka ninaona ni safari nzuri
sana katika miaka 10 ya muziki wa Dbanjo.Dbanjo mwaka jana anasema kuwa ndio
sehemu kuu katika maisha yake yote ya muziki.Alihutubia katika benki ya dunia
Tedex hapo moyo wake uligusa sehemu ya pekee.
Dbanjo muziki umeshamlipa sana sasa hivi anafurahi anapokuwa
balozi wa vijana wengi wa Kinaijeria yuko tayari kujitoa kwa wengine.Naona giza
kwa wasanii wetu wengi ukimwacha Ambwene Yesaya AY ambao wametoka mbali kuweza
kupata nafasi ya kimataifa kueleza muziki wa bongo walikoutoa.
Lady Jay Dee alifika katika anga za kimataifa lakini muda
mfupi tu hakuweza kuendelea kupambana huko.Tunatamani wakongwe wa Bongo Fleva
wanoujua muziki wetu wangekuwa hata watano (5) katika anga za kimataifa
tungeionesha dunia muziki wa bongo fleva ni muziki uliopiganiwa usiku na mchana
kufika hapa.
Inasikitisha hatua zao nyingi zimepotea wakAti tunaziona leo
hii wanakumbuka ya jana,hawaishi kukumbusha walivyoitawaal jana.Simaanishi kuwa
kosa ni lao hapana inawezekana mfumo wa muziki ulikuwa bado hujajengeka.Lakini
bado haitoshi kuacha kuongelea jambo linalogusa kama hili nani hatamani kuona wakongwe
wetu leo hii wakitikisa Duniaa kama Dbanj.
0 maoni:
Chapisha Maoni