#News room
Mkutano wa mawaziri wa fedha kutoka nchi zinazotumia sarafu ya Yuro, ambao ukikua ukijadili hali ya kiuchumi inayojiri nchini Ugiriki ulidumu kwa masaa machache tu Jumatatu Februari 16 na kumalizika bila hata hivyo kufikia maelewano.
Lakini jinsi hali inavyokwenda ndivyo muda uliyotolewa kwa kuikoa Ugiriki unavyofikia kikomo.


Mradi uliyotolewa na nchi zinazotumia sarafu ya Yuro ulionekana na Ugiriki kuwa "haufai" na" haukubaliki", kwani ilikua suala la kuendelea na mpango wa misaada kwa sasa. " Katika mazingira haya, makubaliano yoyote hayawezi kufikiwa kwa leo", Ugiriki imeongeza kusema.



Waziri wa Fedha wa Ugiriki, Yanis Varoufakis, alionya kuwa Ugiriki iko katika hali ya hatari kiuchumi.

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top