Na Hosea Mchopa #UO2

Nimetoka katika klabu kubwa kwenda klabu kubwa .Ni  nafasi ya nzuri kwangu.
Kauli ya Sherwood

Tim Sherwood amechaguliwa kuziba nafasi ya kocha aliyefungishwa virago Paul Lambert  baada ya kutofanya mambo ambayo klabu ya Aston Villa yalitegemea.

Tim Sherewood mwenye miaka 46 ameonekana kuikubali kazihiyo kirahisi mara baada ya kupigiwa simu na siku ya jumamosi alikuwepo kuishuhudia Aston Villa ikimuadhibu Leicer City goli 2-1.
Wachezaji wa Aston Villa wakishangilia ushindi dhidi ya Leicer City


Majukumu ya mwanzoni ya kocha huyu ni kumrejesha mchezaji ambaye Arsenal Wenger alihitaji hudumu yake msimu uliopita Christian Benteke.Benteke ndiye alikuwa roho wa Aston Villa hivi sasa amefinga bao 3 tu katika mechi 19.Katika misimu miwili iliyopita alifunga mabao 34 katika mechi 64.
Mshambualiaji wa Aston Villa Christian Benteke

Timothy Alan Tim Sherwood  alizaliwa February 6 mwaka 1969 .Alikuwa mchezaji katika nafasi ya kiungo toka mwaka 1987 hadi alipostaafu 2005.
Kocha mpya wa Aston Villa Tim Sherwood

Kumbukumbu muhimu za Sherwood.
Alikuwa nahodha wa klabu ya Blackburn Rovers iliyoshinda ubingwa wa ligi kuu ya uingereza mwaka 1995.

Alicheza Watford,Norwich,Spurs,Portsmouth na Coventry city.

Alicheza mechi 3 katika maisha yake ya soka kwa upande wa timu ya taifa ya Uingereza.

Kumbukumbu ya kuvutia

Mechi yake ya mwisho akiwa kocha wa Spurs aliifunga Aston Villa kwa  3-0 mei 11 2014.
16 Feb 2015

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top