Na hosea Mchopa #UO 1
Manchester united walipambana na Preston North Ends katika
mchezo wa FA katika mchezo ambao wenyeji Preston walilala kwa goli 3-1.
Mbele ya
mwamuzi Phil Dowd mashabiki 21,348
walilolipia kiingilio walishuhudi HerreRa dakika ya 65 ,Fellain dakika ya 72 na
nahodha Wayne Rooney ‘WAZA’ dakika ya 82 wakipachika magoli kwa upande wa
united.
Alikuwa ni Laird dakika ya 47 ndiye aliyefungua
kalamu ya magoli na goli pekee kwa Prestoni
Dondoo muhimu za dimbani
Manchester United
walitawala mchezo kwa asilimia 65 kwa 35 za Preston
Pamoja na Preston
kupiga mashuti 14 waliwazidi shuti moja tu Manchester united waliopiga mashuti
11 katika mashuti yaliyolenga golini.Preston walilenga mara 6 wakati united
mara 5.
Kiungo wa Manchester
united Ander Herrera alicheza mechi
yake ya tatu ndani ya miezi mitatu.
4-1-2-2-1 ni moja ya mifumo kocha Van Gaal aliyotumia katika mechi ya Manchester united dhidi ya
Preston North end.
Ilikuwa ni mara ya kwanza tangu mwaka 1972 Manchester united kucheza katika dimba la Preston katika
mchezo wa mashindano.
PAMOJA NA KUFUNGWA
KOCHA WA PRESTON ALITOA KALI YA KIPEKEE
Kocha wa Preston
Simon Grayson
‘Tulitengenza baadhi ya nafasi nzuri katika muda na
wachezaji wanaweza kuamka asubuhi wakijipongeza kwa kitu walichokifanya.
0 maoni:
Chapisha Maoni