Na hosea Mchopa #UO 1

Mbele ya mwamuzi Cuneyt Cakir mashabiki wa soka walishuhudia matukio ya aina yake katika usiku wa mabingwa wa ulaya.Katika mechi kali kati ya Chelsea na Paris Sain German.


Klabu ya matajiri wa ufaransa Psg pamoja na kutawala mchezo kwa asilimia 54 kwa 46 waliambulia sare ya goli 1-1 na Chelsea.

Alikuwa beki wa Chelsea Ivanovic katika dakika ya 36 alipounganisha mpira kwa kichwa na kufunga goli la 5 kwa msimu  huu na kuwapa Chelsea matumaini ya kusonga mbele.

Mchezaji hatari raia wa Psg Edison Cavan alisawazisha goli dakika ya 54 na kufanya matokeo yaishe kwa sare ya goli 1-1.


MAMBO MUHIMU YA KUVUTIA PSG V CHELSEA.
Ibramovic amefunga magoli 7 katika hatua ya mtoano katika mechi 34 alizocheza

Ivanovic jana alifunga goli lake la 1 katika michuano ya ulaya tangu mwaka 2013 alipofunga katika fainali ya ligi ya europa dhidi ya Benfica.
Kocha wa zamani wa Manchester united na David Bekham walikaa karibu kabisa wakitazama mechi hiyo.

Ediso Cavan amefunga magoli 5 katika mechi 6 na kuisaida PSG kufanya vizuri katika hatua ya makundi.

Mtukutu Diego Costa jana alirejea baada ya kuwa nje kwa mechi 3 baada ya kupewa adahabu.

Beki raia wa Brazil mzaliwa wa Diadema David Luiz alicheza  akiwa amevaa jezi ya PSG akitumikia katika nafasi ya kiungo dhidi ya timu yake ya zamani Chelsea
..

Kwa matokeo haya bado yanatoa mwanga kwa pande zote mbili kuelekea mchezo wa marudiano

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top