#news room


Silaha kali za kivita
Silaha kali bado hazijaondolewa kwenye uwanja wa mapambano mashariki mwa Ukraine
Majeshi ya Ukraine na ya waasi wanaoungwa mkono na Urusi bado hawajaziondoa silaha kali kutoka kwenye mpaka wa uwanja wa mapambano mashariki mwa Ukraine. Silaha hizo zilipaswa kuanza kuondolewa leo Jumanne.



Silaha kali za kila upande zilipaswa kuondolewa kuanzia leo kwenye mpaka wa uwanja wa mapambano,kwa mujibu wa makubalinao ya kuyasimamisha mapigano yaliyofikiwa baina ya viongozi wa Ujerumani, Urusi,Ufaransa na Ukraine. Kila upande uliashiria hapo jana kuwa utaziondoa silaha zake ikiwa mwingine nao utafanya hivyo.

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top