Na Hosea Mchopa #UO 1

Mechi hii ilikuwa ni ya mara ya kwanza kwa Suirez kukutana tena na kipa Joe Hart tangu wakutane  Brazil Sao Paulo june 19 .Ambapo Uingereza ilifungwa goli 2-0 na Uruguay huku Suarez akimtungua magoli yote mawili Joe Hart kama alivyofanya jana.
Luis Suarez akishangilia bao lake baada ya kuitungua City


#hii kutoka etihad kwa ajili yako

Mshambuliaji hatari wa klabu ya zamani ya Liverpool Luis Suarez ameweza kuendeleza historia yake ya ufalme kila anapokanyaga  ardhi ya Uingereza baada ya kuifunga Man city wakiwa nyumbani Etihad kwa goli 2-0.


Ilikuwa ni mechi iliyosubiriwa kwa hamu na wapenzi wa soka duniani huku Gerard Pique akiamini ni mechi bora kwa mwaka mpaka sasa.

Ilichukua dakika 16 tu kwa mshambuliaji hatari wa klabu ya Barcelona Luis Suarez kuweza kutikisa nyavu mbele ya kipa Joe Hart.

Luis Suarez akipachika bao la kwanza la Barcelona
Suarez akicheza kwa uzoefu mkubwa dhidi ya timu za uingereza alithibitisha kauli ya kocha Luis Enrique kuwa mchango wake ni mkubwa katika klabu baada ya kupachika bao la pili dakika ya 30.
Luis Suarez akishangilia bao la pili alilofunga akika ya 30


Alikuwa Kun Sergio Aguero dakika ya 69 ndiye aliyeweza kuamsha hisia za mashabiki wa Man city kuwa wanaweza wakasawazisha mechi hiyo.
Sergio Aguero mfungaji pekee wa bao la City alilokwamisha dakika ya 69

Katika Mchezo huo Lionel Messi alikosa penati hivyo kuipa City matumaini ya kuweza kusonga mbele endapo watapambana vyema Camp Nou.
Joe Hart akichza penati ya Lionel Messi


Gael Clichy alienda nje kwa kadi nyekundu na kuipa City wakati mgumu wa kuzuia kasi ya Barcelona.

City mechi ijayo watapata faida kwa kurejea kwa Yahya Toure ambaye anaifahamu klabu ya Barcelona,uwepo wa Silva na mshambuliaji wa daraja la juu Aguero unaweza ukasababisha maajabu yasiyofikirika.

#UO FACT
Suarez alifunga goli moja katika mechi 6 alizokutana na Man City akiwa na jezi za Liverpool..

Sergio Aguero alipiga mashuti mawili tu langoni lakini alifanikiwa kufunga moja.Wakati Edin Dzeko alipiga mashuti 6 bila mafanikio.

Katika mechi 2 za mwisho Suarez alizokutana na Joe Hart amemfunga magoli manne.
Suarez akimtungua Joe Hart akiwa na jezi ya Uingereza nchini Brazil

Luis Suarez akimfunga bao kipa Joe Hart katika mechi ya Uingereza dhidi ya Uruguay nchini Brazil

Sergio Aguero amefunga magoli 11 katika mechi 10 za ligi ya mabingwa  zilizopita




Barcelona katika mechi ya jana walitawala mchezo kwa asilimia 61-39 za Manchester City.Huku wakifanana idadi ya mashuti yaliyolenga golini kila mmoja alipiga mara 9.

24 Feb 2015

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top