Na Hosea Mchopa

Wayne Rooney katika sehemu ya maandalizi yake huwa anakwenda kwa msimamizi maalumu wa vifaa vya michezo.Anamuuliza rangi gani ya jezi tunavaa,kama ni fulana nyekundu,bukta nyeupe na soksi nyeusi au nyeupe.Akishafahamu anaenda kulala na kuvuta picha atakavyofunga goli au kufanya vizuri.

Ni homa ya jiji ambayo haijalishi umekaa upande gani wa jukwaa la uwanja wa taifa da es salaam.Uwe haujavaa rangi ya kijani au nyekundu lakini nawe huugua na huitaji daktari mmoja tu mfumania nyavu.Daktari atakayeleta jeneza uwanjani au atakayewafanya mashabiki waonyeshe ishara ya kuchinja.

 “Ninavutiwa pekee na ufungaji wa mabao .Sikuvutiwa na kitu chochote kingne.Garry Lineker mchezaji wa zamani wa Everton kwenye miaka ya 1985-86 na mtangazaji wa michezo katika kipindi cha Match of the day BBC.Anakata mizizi ya nini watu wanasubiri uwanja wa taifa.

Nani leo kati ya Emmanuel Okwi na Ami Tambwe wanawaza kama Gary Lineker mchezaji pekee aliyetwaa kiatu cha dhahabu katika kombe la dunia mwaka 1986.Vijiwe vingi vya homa ya jiji huwazungumzia wafumania nyavu.Simba wakijitapa na goli zao 5 wakati Yanga wakikumbuka goli 2 .

Mechi ya Simba na Yanga kwa siku za karibuni imekuwa inaenda tofauti kabisa na msemo wa Vince Lombard tulivyo inatokana na nini tunafanya na nini tunacho.Yanga siku za karibuni hata kama ikiwa kwenye kiwango gani ikikutana na Simba ya kawaida inapata tabu sana kupata matokeo.

Isingekuwa roho mkononi kama leo ingekuwa ni mwaka 2003,mashabiki wa Simba wangevaa jezi lao nyekundu siku moja kabla ya mchezo.Hofu ingetoka wapi,golini Juma Kaseja akilindwa na Said Sued,Ramadhan Wasso,Boniface Pawassa na Patric Betwel.

Pluijm anatumia muda mwingi kujiuliza nani awe daktari wa homa ya jiji.Homa ambayo watu wengi wanatamani iwepo hata mara sita kwa mwaka.Anakumbukumbu ya sare pekee alipohatika kupambana dhidi ya Simba mara moja pekee na Simon Muva kumuura dakika za majeruhi.

Pamoja na ubora wa Ndemla kuchezesha klabu ya Simba akisaidiwa na Jonas Mkude katika ukabaji.Fumbo kubwa ni namna gani watahimili mikiki ya Telela na Niyonzima kama wakianzishwa kuweza kumfikihisa mipia Hajjib.Na sio kufikisha tu bali kuleta maafa wanyowaletea katika nani mtani jembe.Nani gani ndemla atafanya maajabu zaidi ya yale ya kuisaidia Simba kurudisha mabao 3 didid ya Yanga.

Bahati ya kipekee ni uwepo wa makocha wazawa ambao wanafahamu homa hii kiundani zaidi.Suleiman Matala akiijua Simba akiwa mchezaji ,kocha wa vijana na novemba 19 2013 akipata nafasi kwa mara ya kwanza kuiongoza timu ya wakubwa baada ya Kibadeni na Julio kutimuliwa.

Je atamuonesha Goran Kopunivich njia bora ya kuwatumia Messi na Okwi ili kutifua mbio za Yanga kileleni.Atampa ushauri gani juu ya nani anastahili kuaminiwa katika safu ya ushambuliaji kwa siku ya leo.
Ni mechi ambayo hatupaswi kumdharau yoyote nani anakumbuka maajabu ya Juma Awadhi aliyoifanya Yanga mtani jembe.Tusije kushangaa leo Maguri akiwasumbua sana Canavaro na Vidic kama wakianza pamoja.

Boniface Mkwasa na yeye ni mtu muhimu kwa klabu ya Yanga uzoefu wake umakini wake kwa wachezaji unaweza ukampa nafasi ya kuipa yanga matokeo.Chicharito akiwa Manchester united siku zote huwa hakosekani mechi dhidi ya Chelsea hata awepo nje kwa muda gani.

Mkwasa ni mtu pekee anayeweza kumuonyesha Pluijm kijana Jeryson Tegete kuwa ni mwiba mkali kwa Simba amefuga karibu mabao 5 alipowavaa.Ijapokuwa hayupo vizuri siku za karibuni.Uwepo wa Mkwasa unaweza ukaleta ladha zisizotarajiwa kwa kumpa  nafasi kijana ngangari Hussein Javu.

Homa hii ya jiji huboresha mikataba na pia huaribu mikataba.Tanzania hamna soka la kweli ni Simba na Yanga wakati pekee tunapoamini sisi ni wa kwanza Afrika Mashariki.Mapato yanakuwa mengi,ndio mechi wachezaji wanapewa marupurupu.

Haya yote yanafanywa kwa lengo moja tu kupata tiba ya homa la jiji,wanataka mabao yatakayoamsha hali ya klabu.Simba ikishika nafasi ya nne na kuhitaji ushindi kuanza kukimilia kileleni.Wakati Yanga wakihitaji pointi 3 kujihakikishia ushindi wa vita yao dhid ya Azam na Kagera Sugar.


Wametafuta fukwe nzuri zenye utulivu wakijifua Zanzibar na Bagamoyo kwa kuwa wanafahamu hii ni mechi itakayoleta homa katika klabu zao.Homa inayosambaa jiji nzima na hakuna tiba inayohitajika zaidi ya kutikisa wavu mara nyingi kuliko mwenzako.


0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top