Na Hosea Mchopa #UO 1
4-3 ni pumzi inayoshikilia soka kwa hivi sasa.Unajua kwa
namna gani Messi akichungulia gazeti la michezo la Marca akiiona 4-3 anavyowaza
kuongeza juhudi.Je umewahi kuwaza kijana wa Madeira Cristiano Ronaldo
anavyowaza kuipigania.
Pumzi zao zimetikiswa na binadamu aliye na damu ya kibrazili.Nchi iliyobarikiwa
warembo wenye majina ya kuvutia Ana Amelia,Ana Lucia,Ana Livia,Alidaci.Turudi
kwenye mstari wetu.
Huyu ni mkongwe mwenye miaka 74 aliyechaguliwa na shirikisho
la takwimu na historia ya soka (IFFHS)kuwa mchezaji bora wa karne mwaka 1999.
![]() |
Perola Negra O Rei Pele |
Huyu si mwingine ni Edson Arantes do Nasciamento ‘ O Rei Pele’
au Perola Negra anaposahau kumweka
Ronaldo daraja moja na Booby Moore,Boby Charton na George Best.Kamweka Messi tu
tena na wakongwe kama Zico na Rivaldo.
Kauli ya Pele juu ya Ronaldo na Messi huwa na nguvu ya aina
yake katika ulimwengu wa soka.Kumbuka Pele ni mchezaji anayeheshimika kwa
kutupia magoli 1281 katika mechi 1363.
Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wapo kwenye ulimwengu wa
ushindani mkubwa katika soka.Ulimwengu wao unaanza ndio unafuta wa
Suarez,Neymar,Bale,Benzema,Aguero,Rooney na wengine.
Hivi sasa dunia nzima inageukia nchi ya Hispania kuangalia
wanaume wakipambana katika mechi yenye mvuto kwa sasa El Classico.Mechi ambayo
inatoa hamasa kubwa sana katika mbio za ubingwa ukizngatia wao ndio washindani
wakuu.
![]() |
Cristiano Ronaldo CR7 |
Cristiano Ronaldo alianza msimu huu kwa hamasa kubwa na ya
kutisha baada ya kufunga mabao 25 katika mechi 14.Lakini Tangu mwaka 2015 uanze
amekuwa chini ya kiwango kwani michezo minne ndani ya mwaka huu alishindwa
kupiga shuti lilolenga kwenye goli.Na amefunga mabao 5 tu.
Mwaka 2015 umeharibu rekodi yake aliyoweka miezi 15 iliyopita ya kufunga michezo ya
Bernabeu.Ilikuwa katika mchezo dhidi ya Espanyol walishinda bao 3-0 lakini
Ronado hakufunga bao lolote.
Kuna taarifa kuwa Ronaldo anatarajiwa kukwepa vyombo vya
habari ili kuendelea kutuliza akili.Kwani vyombo vingi vimekuwa vikihitaji
kumchomekea swali la mahusiano yake na Irina Shayk.Ambaye tayari amechafua hali
ya hewa baada ya kusema kilichosababisha aachane naye kupitia Holla magazine.
Msumari wa Pele unaweza ukawa umetikisa pumzi na hasira za
Ronaldo kutaka kuonesha ulimwengu kuwa yeye ni bora.Naye Lionel Messi pumzi
zake zitatikiswa na mafanikio ya Ronaldo kwa kuhitaji kufanya zaidi.Ili
kushindana katika kuongeza ballon dor ya
5.
Lionel Messi katika mechi 17 za Barcelona ametupia magoli 20
na akitoa pasi za goli 12 akikimbia kwa kasi ya ajabu mwaka 2015.
Pia Lionel Messi amepata nguvu ya ajabu kutokana na maelewano
mazuri yaliyopo kati yake na wachezaji wenzake Neymar Jr na Luis Suarez.Huku
Madrid hali ya Gareth Bale na Ronaldo ikiwa si shwari kwa kulaumiana juu ya
ubinafsi.
![]() |
Lionel Mess La Pulga |
Akiwa na hali ya ajabu na klabu kiujumla wakiwa wameshinda
mechi 9 kati ya 10 zilizopita.Kauli ya Pele itakuwa imetikisa pumzi zake na
anajua anatakiwa kujitahidi zaidi kabla ya Ronaldo hajarudi katika kiwango
chake.
Pele amechochea moto wa Ronaldo kuhitaji kuchukua tuzo ya
Ballon Dor a 4 hili iwe 4-4.Kuelekea mchezo huu hakuna anachohitaji zaidi
ya kufanya maajabu.
Kama Ronaldo ataisadia klabu yake kushinda dhidi ya Barcelona
atakuwa ameishuhudia rekodi ya aina yake.Real Madrid mara mwisho kushinda mechi
3 mfululizo dhidi ya Barcelona ilikuwa ni mwaka 1978.
Ronaldo amefunga mabao 8 katika michezo 7 waliyosafiri kwenda
Nou Camp.Je atatamba tena mbele ya Messi.Au mechi hii itamtengenisha kabisa na
mashabiki wa Madrid waliompigia kura awe anaanzia benchi.
Pamoja na kuhitaji ushindi wa pointi 3 za kuwezesha klabu zao
kuendeleza vita za kuchukua la liga.Hakuna siri Ronaldo na Messi wapo katika
mashindano ya tuzo ya mchezaji bora wa dunia.Messi akiwa ana tuzo 4 na Ronaldo
3(4-3).
Perola Negra hajafanya kosa ametikisa pumzi zao mapema kabla
ya El Classico.Hakuna asiyehitaji kuona El Classico inakuwa mechi ya Ronaldo au
Messi.Uso huwa mkali chuki ikitanda njia moja tu ya kuleta tabasamu ni
mafanikio.Ni la Pulga (Messi ) au CR7 (Ronaldo).
0 maoni:
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.